Pata taarifa kuu

Gaza: Wanawake na watoto zaidi ya Elfu Moja kupokea matibabu barani Ulaya

Wanawake na watoto karibia Elfu Moja wanaohitaji huduma za kimatibabu wanatarajiwa kuondolewa katika Ukanda wa Gaza na kupelekwa barani Ulaya kutibiwa, kwa mujibu wa WHO barani Ulaya.

Israeli imendelea kutekeleza mashambulio dhidi ya vituo vya afya katika Ukanda wa Gaza kwa mujibu wa WHO.
Israeli imendelea kutekeleza mashambulio dhidi ya vituo vya afya katika Ukanda wa Gaza kwa mujibu wa WHO. © Omar al-Qataa/AFP
Matangazo ya kibiashara

Taarifa ya Hans Kluge, afisa kutoka shirika la WHO bara Ulaya, inasema mpango huo utaoongozwa na WHO pamoja na mataifa mengine ya EU yanayohusika kwenye shuguli hiyo.

Siku ya Alhamis, wataalam wa uchunguzi kutoka Umoja wa Mataifa katika ripoti yao, walithibitisha kwamba Israeli inalenga kimakusudi vituo vya afya katika Ukanda wa Gaza.

Raia wa Palestine akiwa karibu na vifusi vya jengo kufuatia shambulio la Israeli huko Khan Yunis kusini mwa Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 17, 2023.
Raia wa Palestine akiwa karibu na vifusi vya jengo kufuatia shambulio la Israeli huko Khan Yunis kusini mwa Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 17, 2023. © Mahmud HAMS / AFP

Ripoti hiyo aidha ilieleza kwamba wanajeshi wa Israeli kando na kushambulia vituo vya afya pia inawatesa wahudumu wa afya na kuwaua wengine.

Vilevile ripoti hiyo ya UN pia iliituhumu Israeli kwa kutekeleza makosa ya uhalifu wa kibinadamu.

Raia wa Palestine wakimbeba mwenzao aliyejeruhiwa katika shambulio katika Ukanda wa Gaza eneo la  Khan Younis. Desemba 1 2023.
Raia wa Palestine wakimbeba mwenzao aliyejeruhiwa katika shambulio katika Ukanda wa Gaza eneo la Khan Younis. Desemba 1 2023. © Saher ALGHORRA for AP/Zuma Press

Rik Peeperkorn, mwakilishi wa WHO katika maeneo yanayokaliwa na raia wa Palestine, mwezi Mei alieleza kwamba karibia watu Elfu 10 walikuwa wanahitaji kuondolewa kwa dharura katika Ukanda wa Gaza kwa ajili ya matibabu.

Shirika la WHO ukanda wa bara Ulaya tayari limewasaidia watu 600 wanaohitaji matibabu kuondoka katika Ukanda wa Gaza na kuwapeleka katika mataifa saba ya EU tangu kuzuka kwa mapigano mwezi Oktoba mwaka wa 2023.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.