Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Msaada wa Kibinadamu

Picha ya maktaba: Bruno le Marquis, mwakilishi wa katibu mkuu na mratibu wa UNOCHA nchini DRC akizungumza mbele ya waandishi kambini Bulengo.
UN News/Byobe Malenga

Kusimamishwa kwa msaada wa Marekani kumeathiri operesheni za kibinadamu DRC

Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Bruno Lemarquis, leo (11 Feb) ameeleza kwamba uamuzi wa serikali ya Marekani kusimamisha msaada wa kigeni “ni chanzo kikubwa cha wasiwasi,” kwani mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa na mengine yasiyo ya kimataifa yanayofanya kazi mashinani yameathirika vibaya, kama sio kusitisha kabisa shughuli zao.

Watoto wakikusanyika katika jengo lililoharibiwa huko Al Nuseirat, katikati mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Majira ya baridi yakiendelea Gaza, wahudumu wa kibinadamu wataka fursa zaidi kufikisha misaada: UN

Wakati jeshi la Israeli lilipomaliza kujiondoa mwishoni mwa wiki kutoka kwenye ukanda muhimu wa usalama huko Gaza ambao ulikuwa umekata eneo hilo katika sehemu mbili, mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yametoa ombi jipya la kukomeshwa kwa vikwazo vyote vya misaada ambavyo vinaendelea kuzuia utoaji wa msaada wa kuokoa maisha.

Huko Kakuma nchini Kenya wakimbizi wafuga nyenje au Crickets ambazo ni chanzo cha protini.
WFP Video

Je, unafahamu kwamba nyenje ni chanzo cha protini?

Katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma, kutokana na ufadhili wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), kundi la vijana wanajishughulisha na ufugaji wa wadudu nyenje (Crickets) ili kukabiliana na changamoto ya utapiamlo miongoni mwa watoto wachanga. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Sauti
1'32"
Vikosi vya kwanza vya Ghana vilivyotumwa kama sehemu ya operesheni ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa kusaidia kurejesha utulivu nchini Jamhuri ya ya Congo ya zamani (ONUC). Pichani ni polisi wa Ghana mwezi August mwaka 1960 wakiwa mjini Leopoldville am
UN Photo/HP

Kwa nini walinda amani wa Umoja wa Mataifa wamekuwa DRC kwa miaka 65?

Historia ya nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), imeangaziwa na vita vikali vinavyohusishwa na ukosefu wa utulivu wa kisiasa wa kitaifa, mwingiliano wa migogoro ya kikanda, na unyonyaji wa maliasili nyingi za taifa hilo la Afrika ya Kati. Tangu uhuru wa nchi hiyo mwaka 1960, Umoja wa Mataifa umeleta manufaa sana nchini DRC, ikiwa ni pamoja na kutumwa kwa operesheni tatu za amani ambazo kwa upande wake zimechagiza shughuli za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa katika kipindi cha miaka 65 iliyopita.

Msongamano wa magari unarejea katika mitaa ya Goma baada ya ukosefu wa usalama wa hivi majuzi.
UN News

Janga la afya Mashariki mwa DRC lataka juhudi zaidi za WHO

Kuongezeka kwa ghasia za hivi majuzi huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumesababisha hasara kubwa ya maisha, kiwewe, kuhama makazi, na uharibifu wa miundombinu muhimu ya afya, na kuzidisha hali ambayo tayari ni mbaya kwa mamilioni ya watu. Hali imebaki kuwa ya wasiwasi na tete, na mahitaji ya afya ni makubwa, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO leo jijini Geneva, Uswisi.